TCU Majina 9890 ya Waliochaguliwa Chuo zaidi ya Kimoja awamu ya tatu 2024/2025

Filed in Education by on 19/10/2024 0 Comments
TCU Majina 9890 ya Waliochaguliwa Chuo zaidi ya Kimoja awamu ya tatu 2024/2025

TCU Majina 9890 ya Waliochaguliwa Chuo zaidi ya Kimoja awamu ya tatu 2024/2025, Majina ya waliochaguliwa chuo zaidi ya kimoja awamu ya tatu PDF.

Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) inaufahamisha umma, Taasisi za Elimu 
ya Juu na wadau wa Elimu ya Juu ndani na nje ya nchi kuwa udahili katika awamu ya Tatu na ya mwisho kwa ngazi ya Shahada ya Kwanza katika Taasisi za Elimu ya Juu nchini kwa mwaka wa masomo 2024/2025 
umekamilika.
Majina ya waliodahiliwa katika Awamu ya Tatu yametangazwa na vyuo husika.
WAOMBAJI WALIODAHILIWA KATIKA CHUO ZAIDI YA KIMOJA
Waombaji waliodahiliwa katika chuo zaidi ya kimoja katika awamu ya tatu na 
wale ambao hawakuweza kuthibitisha udahili katika awamu zilizopita, 
wanapaswa kuthibitisha udahili wao katika chuo kimojawapo kuanzia leo
tarehe 19 hadi 21 Oktoba, 2024.
Uthibitisho huo unafanyika kwa kutumia 
namba maalum ya siri iliyotumwa kwa ujumbe mfupi kupitia namba zao za 
simu au barua pepe (email) walizotumia wakati wa kuomba udahili.
Wale ambao hawatapata kwa wakati ujumbe huo, wanashauriwa kuingia kwenye mifumo ya udahili ya vyuo walivyodahiliwa na kuomba kutumiwa ujumbe mfupi wenye namba maalum ya siri ili kuweza kujithibitisha katika chuo husika. 
Aidha, uthibitisho wa udahili ufanyike kupitia akaunti ambayo muombaji 
alitumia wakati wa kuomba udahili.
Kwa urahisi wa rejea, orodha ya majina 
ya waliodahiliwa katika chuo zaidi ya kimoja inapatikana kwenye tovuti ya 
TCU (www.tcu.go.tz). 
WITO KWA WAOMBAJI UDAHILI
Waombaji udahili wa Shahada ya Kwanza wanakumbushwa kuwa masuala 
yote yanayohusu udahili au kujithibitisha katika chuo kimoja yawasilishwe 
moja kwa moja kwenye vyuo husika.
Kwa wale ambao watapata changamoto 
katika kujithibitisha, vyuo vyote vimeelekezwa kupokea taarifa zao na 
kutafuta ufumbuzi wa haraka kwa kuzingatia miongozo na taratibu 
zilizowekwa.

Orodha ya waombaji waliodahiliwa zaidi ya Chuo kimoja au Program zaidi ya moja katika awamu ya tatu ya udahili na wale ambao hawakuthibitisha awamu zilizopita kwa mwaka wa masomo 2024/2025 imeambatanishwa kwenye PDF hapa chini;

MATANGAZO YA KAZI BOFYA HAPA

JIUNGE NA GROUP LETU HAPA, JIUNGE NA CHANNEL YETU HAPA, JIUNGE NA TELEGRAM HAPA.


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error: Content is protected !!