MMOJA akutwa na Virusi vya Marburg Kagera

MMOJA akutwa na Virusi vya Marburg Kagera
MMOJA akutwa na Virusi vya Marburg Kagera
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema mtu mmoja amekutwa na maambukizi ya virusi vya Marburg (MVD) Wilayani Biharamuro, Mkoani Kagera baada ya taarifa kusambaa mitandaoni kwamba kuna ugonjwa wa virusi vya Marburg Mkoani humo.
Dkt. Samia ameyasema hayo leo January 20, 2025, wakati akizungumza na waandishi wa habari alipotembelewa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Dkt Tedros Ghebreyesus Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma.
Hayo yanajiri siku sita tangu WHO iweke wazi kuhusu watu nane kufariki Dunia kutokana na ugonjwa unaoshukiwa kuwa wa virusi vya Marburg mkoani humo ambapo January 11, Serikali ilituma timu ya wataalamu mkoani humo na kufanya uchunguzi ambapo katika sampuli zilizochukuliwa ni mgonjwa mmoja pekee aliyekutwa na maambukizi hayo.
