KALENDA ya Mihula ya Masomo 2025
KALENDA ya Mihula ya Masomo 2025
WARAKA WA ELIMU NA. 02 WA MWAKA 2024 KUHUSU KALENDA YA MIHULA YA MASOMO KWA SHULE ZA AWALI, MSINGI NA SEKONDARI MWAKA 2025
Kwa kuzingatia umuhimu wa kuwa na idadi sahihi ya siku za masomo, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imeandaa Kalenda ya Mihula ya Masomo kwa Shule za Awali, Msingi na Sekondari kwa mwaka wa masomo 2025.
Ni muhimu kuzingatia utekelezaji wa Kalenda husika kwa ufanisi ili kuepuka changamoto ya kutokamilisha ufundishaji na ujifunzaji wa mada zote kwa wakati na hivyo kulazimika kuweka mipango ya ufundishaji na ujifunzaji inayowanyima watoto/wanafunzi fursa ya kupumzika na kushiriki kikamilifu katika shughuli za kijamii katika familia na jamii zao.
Kalenda ya Mihula ya Masomo kwa Shule za Awali, Msingi na Sekondari kwa mwaka 2025 ni kama ifuatavyo:

KALENDA ya Mihula ya Masomo 2025
Tanbihi:
Siku za Masomo kwa mwaka ni 194.
Mashindano ya UMITASHUMTA yatafanyika tarehe 08/06/2025 hadi 21/06/2025, na UMISSETA yatafanyika tarehe 22/06/2025 hadi 04/07/2025.
Mashindano ya Michezo ya Shule za Sekondari za Afrika Mashariki (FEASSSA)
yatafanyika tarehe 17/08/2025 hadi 29/08/2025.
