FOMU za Kujiunga na Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA)

Filed in Education by on 15/10/2024 0 Comments

FOMU za Kujiunga na Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA)FOMU za Kujiunga na Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA)

VETA imeweka utaratibu maalum kwaajili ya kujiunga ili kupata mafunzo katika vyuo inavyovimiliki. Utaratibu ni kama unavyoelezwa hapa chini:

MATANGAZO YA KAZI BOFYA HAPA

VETA hutoa mafunzo ya muda mrefu na mfupi na katika mifumo mbalimbali.

Kwa mafunzo ya muda mrefu, yyuo vyote hutangaza nafasi za kujiunga mwezi wa Agosti kila mwaka. Matangazo hutolewa katika vyombo vya habari nchini pamoja na kwenye tovuti ya www.veta.go.tz

Mwombaji ni lazima awe amemaliza elimu ya msingi, sekondari na kuendelea.

Mwombaji ni lazima awe amemaliza elimu ya msingi, sekondari na kuendelea.

Mwombaji huchukua fomu katika chuo chochote kilichopo karibu. Fomu hizo zina taarifa ya vyuo vyote vinavyomilikiwa na VETA, ikiwa ni pamoja na fani zinazofundishwa na mahali chuo kilipo na kama ni kutwa au bweni.

Mwombaji anaruhusiwa kufanya mtihani wa kujiunga mkoa aliochukua fomu lakini anaweza kuchagua kusoma mkoa wowote anaochagua kulingana na mahitaji yake.

Mwombaji anatakiwa kufanya mtihani wa kujiunga (Aptitude Tests) mwezi Oktoba na wale wanaofanikiwa kuchaguliwa hupewa taarifa mwezi Decemba ili kuanza masomo Januari mwaka unaofuata.

Mwombaji anayefanikiwa hupewa barua ya kujiunga inayofafanua mahitaji yote muhimu. Mahitaji yanatofautiana toka chuo kimoja hadi kingine na kutegemeana na fani aliyoomba, na pia kama ni kutwa au bweni.

Kwa utaratibu huu Mwombaji anaanza kujiunga na daraja la 1(Level 1) ambalo ni daraja la chini. Waombaji wanaoendelea madaraja ya juu (Level II-III) vigezo ni ufaulu wa daraja husika unamwezesha kupanda daraja lingine.

Ada na gharama za mafunzo kwa vyuo vinavyomilikiwa na VETA.
Ada za mafunzo kwa kozi za muda mrefu kwa vyuo vinavyomilikiwa na VETA kwa sasa ni shilingi 60,000/= kwa mwanafunzi wa kutwa katika fani zote na bweni ni shilingi 120,000/=.
Mahitaji mengine hutegemeana na fani na chuo, yanakadiriwa kuwa kati ya Shilingi 200,000 na 250,000.
MAMLAKA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI STADI FOMU ZA MAELEZO YA KUJIUNGA KATIKA VITUO VYA UFUNDI STADI MWAKA 2024.
Waombaji walio karibu na vituo walivyochaguliwa, wanaweza kufika katika vituo hivyo ili kupatiwa fomu zenye maelezo ya kujiunga.

JIUNGE NA GROUP LETU HAPA, JIUNGE NA CHANNEL YETU HAPA, JIUNGE NA TELEGRAM HAPA.


Tags:

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error: Content is protected !!